1
Yn 3:16
Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Bandingkan
Selidiki Yn 3:16
2
Yn 3:17
Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.
Selidiki Yn 3:17
3
Yn 3:3
Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.
Selidiki Yn 3:3
4
Yn 3:18
Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
Selidiki Yn 3:18
5
Yn 3:19
Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.
Selidiki Yn 3:19
6
Yn 3:30
Basi hii furaha yangu imetimia. Yeye hana budi kuzidi, bali mimi kupungua.
Selidiki Yn 3:30
7
Yn 3:20
Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.
Selidiki Yn 3:20
8
Yn 3:36
Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia.
Selidiki Yn 3:36
9
Yn 3:14
Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa
Selidiki Yn 3:14
10
Yn 3:35
Baba ampenda Mwana, naye amempa vyote mkononi mwake.
Selidiki Yn 3:35
Halaman Utama
Alkitab
Pelan
Video