1
Luka 17:19
Swahili Revised Union Version
Akamwambia, Inuka, nenda zako, imani yako imekuokoa.
Kokisana
Luka Luka 17:19
2
Luka 17:4
Na kama akikukosea mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Luka Luka 17:4
3
Luka 17:15-16
Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu; akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
Luka Luka 17:15-16
4
Luka 17:3
Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.
Luka Luka 17:3
5
Luka 17:17
Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale tisa wako wapi?
Luka Luka 17:17
6
Luka 17:6
Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng'oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.
Luka Luka 17:6
7
Luka 17:33
Mtu yeyote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na yeyote atakayeiangamiza ataiponya.
Luka Luka 17:33
8
Luka 17:1-2
Akawaambia wanafunzi wake, Vikwazo havina budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye vinakuja kwa sababu yake! Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.
Luka Luka 17:1-2
9
Luka 17:26-27
Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu. Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
Luka Luka 17:26-27
Ndako
Biblia
Bibongiseli
Bavideo