1
Yohane 15:5
Biblia Habari Njema
“Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami nikiwa ndani yake, huyo huzaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
Összehasonlít
Fedezd fel: Yohane 15:5
2
Yohane 15:4
Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Kama vile tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipobaki katika mzabibu, hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
Fedezd fel: Yohane 15:4
3
Yohane 15:7
Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
Fedezd fel: Yohane 15:7
4
Yohane 15:16
Nyinyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapeni chochote mnachomwomba kwa jina langu.
Fedezd fel: Yohane 15:16
5
Yohane 15:13
Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
Fedezd fel: Yohane 15:13
6
Yohane 15:2
Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda yeye huliondoa, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
Fedezd fel: Yohane 15:2
7
Yohane 15:12
Hii ndiyo amri yangu: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi.
Fedezd fel: Yohane 15:12
8
Yohane 15:8
Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
Fedezd fel: Yohane 15:8
9
Yohane 15:1
“Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
Fedezd fel: Yohane 15:1
10
Yohane 15:6
Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
Fedezd fel: Yohane 15:6
11
Yohane 15:11
Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
Fedezd fel: Yohane 15:11
12
Yohane 15:10
Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
Fedezd fel: Yohane 15:10
13
Yohane 15:17
Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: Pendaneni.
Fedezd fel: Yohane 15:17
14
Yohane 15:19
Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda nyinyi kama watu wake. Lakini kwa vile nyinyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
Fedezd fel: Yohane 15:19
Kezdőoldal
Biblia
Tervek
Videók