Walipokwisha kula, Yesu akamwuliza Simoni Petro: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda mimi kuliko hawa?”
Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!”
Yesu akamwambia: “Tunza wana-kondoo wangu.”
Akamwuliza tena mara ya pili: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?”
Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!”
Yesu akamwambia tena: “Chunga kondoo wangu.”
Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?”
Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!”
Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.