1
Mathayo 7:7
Swahili Revised Union Version
Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa
Compare
Explore Mathayo 7:7
2
Mathayo 7:8
kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.
Explore Mathayo 7:8
3
Mathayo 7:24
Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba
Explore Mathayo 7:24
4
Mathayo 7:12
Basi yoyote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo Torati na Manabii.
Explore Mathayo 7:12
5
Mathayo 7:14
Bali mlango ni mwembamba, na njia imebana iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
Explore Mathayo 7:14
6
Mathayo 7:13
Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.
Explore Mathayo 7:13
7
Mathayo 7:11
Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu zawadi njema, je! Si Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema zaidi wao wamwombao?
Explore Mathayo 7:11
8
Mathayo 7:1-2
Msihukumu, msije mkahukumiwa ninyi. Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa.
Explore Mathayo 7:1-2
9
Mathayo 7:26
Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga
Explore Mathayo 7:26
10
Mathayo 7:3-4
Basi, mbona wakitazama kibanzi kilicho ndani ya jicho la ndugu yako, na boriti iliyo ndani ya jicho lako mwenyewe huioni? Au utamwambiaje nduguyo, Niache nikitoe kibanzi katika jicho lako; na kumbe! Mna boriti ndani ya jicho lako mwenyewe?
Explore Mathayo 7:3-4
11
Mathayo 7:15-16
Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya kondoo, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali. Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?
Explore Mathayo 7:15-16
12
Mathayo 7:17
Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
Explore Mathayo 7:17
13
Mathayo 7:18
Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
Explore Mathayo 7:18
14
Mathayo 7:19
Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
Explore Mathayo 7:19
Home
Bible
Plans
Videos